Mabingwa
Watetezi na Vinara wa VPL, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania, Yanga Leo
wamezidi kujongomea juu kileleni baada ya kutoka nyuma kwa Bao 1-0 na
kuichapa Toto African 2-1 huko CCM Kirumba, Mwanza.
Toto
walitangulia kuifunga Yanga kwa Bao la Dakika ya 39 la William Kimanzi
na Yanga kupiga Bao 2 Kipindi cha Pili Dakika za 50 na 78 Wafungaji
wakiwa Deus Kaseke na Juma Abdul.
Ushindi
huu umeifanya Yanga izidi kupaa kileleni ikiwa na Pointi 65 kwa Mechi
26 ikifuatiwa na Azam FC yenye Pointi 58 na Simba 57 ambao wamecheza
Mechi 25 na Kesho Jumapili wanapambana Uwanja wa Taifa Jijini Dar es
Salaam
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni