Jumatano, 26 Oktoba 2016

YANGA YAIVURUGA JKT RUVU

Siku moja baada ya kocha mkuu wa Dar es salaam young Africa kujiuzulu leo hii likizo hicho kimeondoka na ushindi wa goli nne kwa bila dhidi ya JKT RUVU maafande hawa toka mkoani pwanii. Shukrani zimwendee obrey chirwa aliendelea kuzifumania nyavu pia supersub amisi tambwe akiingia kipindi cha Pili akifunga magoli mawili na saimon msuva akafunga moja.Kwa mchezo huyo simba wanaongoza kwa pointi 29 yanga wanafuatia kwa point 24..

VIKWAZO VYA UJASILIAMALI

Ujasiliamali ni nguzo muhimu katika maendeleo ya watu Popote duniani. Hii ni sekta muhimu ambayo inawezakuleta ajira ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja kwa watu hasa vijana. Kwa Nchi zinazoendelea hasa za Africa sekta hii ni muhimu sana ili kupunguza tatizo la ajira kwa vijana. Nchi nyingi za Africa ina namba kubwa ya vijana wasio na kazi ambapo hupelekea vijana kujiunga na delta zisizo rasmi ili wapate pesa za haraka na kukidhi mahitaji Yao. Je ni nini changamoto zinazowakabili?
  • Kukosekana.kwa mitaji: hili ni.tatizo sugu amabalo hufanya watu wengi washindwe kwenye sekta ya ujasiliamali. Bank na taasisi za kifedha zimekuwa zinatoa masharti magumu ili kupata Mtaji kama uwe na kiwanja ,nyumba na kadhalika.
  • Elimu duni ya ujasiliamali inachangia wale wanothubutu kushindwa kufikia malengo au mafanikio kwa sababu ya elimu duni au mazoea pia ugumu wa maisha hupelekea biashara kutofanikiwa.
  • Starehe vijana wengi wanakumbwa na nanga la.kupenda starehe hivyo hupelekea kipato kuishi kwenda kumbi za starehe , bar na kwenye majumba ya kulala wageni

Jumatano, 12 Oktoba 2016

CHANGAMOTO ZA KILIMO KWA WAKULIMA

Tanzania ni Nchi iliyojaliwa mabonde na ardhi yenye rutuba. Nchi ambayo ina mito mingi mikubwa kama rufiji,malalasi,ruaha n.k pia kuna maziwa makubwa kama Victoria,Nyasa na Tanganyika, hivyo inawezekana kwa kiasi kikubwa shughuli za kilimo zikafanyika mwaka Mzima. Ila wakulima wamekuwa wakipata changamoto nyingi sana ambazo ni:-

  • PEMBEJEO KUCHELEWA AU KUKOSEKANA
      Wakulima wamekuwa wakisotea kupata pembejeo toka serikalini ambapo kwanza hazifiki kwa wakati na zikifika zinakuwa chache kiasi kwamba watu wachache ndo wanaopata. Hili limeshamili sana vijijini huko ambapo wananchi wanalalamika sana suala hili
  • UKOSEFU WA SOKO LA MAZAO
Bei ya mazao imekuwa gonjwa sugu kwani wanunuzi  wamekuwa wakijipangia bei ya kununua mazao bila kujali upande wa mkulima. Hili suala linapelekea mpaka wakulima wanakata tamaa ya kulima mashamba makubwa wakihofia hasara ambayo wanaweza kupata.  Bado matumizi ya jembe la Mkono yanaendelea na kilimo cha kisasa watu wachache sana ndo wanafanya. Hii hupelekea mavuno machache na mazao yasiyo bora.
  • MATUMIZI YA ZANA DUNI ZA KILIMO

Jumamosi, 4 Juni 2016

BONDIA BINGWA WA MIAKA YA 60 AFARIKI DUNIA

Aliyeluwa bondia wa kwanza maarufu mweney asili ya Kiafrika, Muhammud Ali, wa Marekani amefariki leo asubuhi akiwa na umri wa miaka 74.
Kulingana na msemaji wa familia yake, bingwa huyo wa zamani wa uzani wa juu, anayejulikana sana kote duniani kwa sababu ya machachari yake katika ngumi, alifariki katika jiji la Phoenix Arizona, baada ya kulazwa hospitalini Alhamisi.
Alikuwa na matatizo ya kupumua, hali ambayo ilitatanishwa zaidi na maradhi ya Parkinson, ambayo ni hali ya mgonjwa kutetemekatetemeaka.
Taarifa ya familia yake imesema kuwa ibada ya mazishi itafanywa nyumbani kwake Lousville, Kentucky.

Jumamosi, 30 Aprili 2016

MATOKEO LIGI KUU VODACOM LEO TAREHE 30/05/2016

Mabingwa Watetezi na Vinara wa VPL, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania, Yanga Leo wamezidi kujongomea juu kileleni baada ya kutoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuichapa Toto African 2-1 huko CCM Kirumba, Mwanza.
Toto walitangulia kuifunga Yanga kwa Bao la Dakika ya 39 la William Kimanzi na Yanga kupiga Bao 2 Kipindi cha Pili Dakika za 50 na 78 Wafungaji wakiwa Deus Kaseke na Juma Abdul.
Ushindi huu umeifanya Yanga izidi kupaa kileleni ikiwa na Pointi 65 kwa Mechi 26 ikifuatiwa na Azam FC yenye Pointi 58 na Simba 57  ambao wamecheza Mechi 25 na Kesho Jumapili wanapambana Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam

MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA ZAHARIBU MIUNDOMBINU YA BARABARA

Kufuatia Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Mtwara zimesababisha wasafiri wanaofanya safari kati ya wilaya ya Tandahimba, Newala, na Dar es Salaam kupata adha kubwa ya usafiri kutokana na barabara kuharibika na kulazimika Magari kuvutwa na Scaveta zinazofanya kazi ya kupunguza mlima kinombedo uliopo wilaya ya Tandahimba.
Wakiwa katika jitihada za kuvuka mlima Kinombedo ambao licha ya kuwepo kwa lami udongo unaoporomoka kutoka juu ya mlima huo umekuwa ukisababisha utelezi na magari kushindwa kupanda mlima ambapo awali madereva wanaoendesha mashine za kuchimbia udongo walishindwa kutoa msaada na kulazimu madereva kuanza kuchimba barabara hali ambayo ilisababisha foleni kubwa zaidi kutokana na malori kuziba njia.
Baada ya jititihada zao kugonga mwamba na kusababisha foleni ya malori ya mizigo pamoja na mabasi ya abiria, Kampuni inayopunguza mlima chini ya msimamizi wake Bw. Haji Abubakari ambaye hakutaka kutaja jina la kampuni inayofanya kazi ilitoa msaada wa kuyavuta magari hayo ambayo baadaye yaliendelea na safari zake , Lakini bwana Haji amesema eneo hilo linapunguzwa mlima ili kuwezesha magari kupita kwa urahisi.
Wakiongea na Safari redio baadhi ya madereva wanaofanya safari zao kati ya Wilaya ya Tandahimba, Newala na Dar es Salaam wameilalamikia serikali ya Mkoa kwa kushindwa kujenga barabra hiyo kwa kiwango cha lami licha ya kuwa imekuwa ina uhitaji mkubwa kwa wananchi wanaoishi na wanaosafiti katika wilaya hizo.
Mmoja wa madereva hao aliyejitambulisha kwa jina na Charles Paulo amesema mara nyingi kipindi cha mvua kumekuwa kukijitokeza kero ya uharibifu wa barabara ambayo kwa namna moja au nyingine imekuwa ikichangia uchakavu wa vyombo vya moto ambavyo vimekuwa vikipita katika barabara hiyo.
Wiki iliyopita Serikali kupitia bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilisema imetenda fedha zaidi ya shilingi Milion 1000 kwa ajili ya kukarabati miundombinu ya barabara na kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayounganisha Mkoa wa Mtwara na Viunga vyake.Kuhu ikidai kuwa serikali kupitia wakala wa barabara Tanroads tayari imesaini mkataba na mkandarasi kutoka Botswana.

AINA ZA WANAWAKE MICHEPUKO

  1. MCHEPUKO LAMI: Huu ni ule ambao hauombi pesa, katulia hana mapepe, uwe naye au usiwe naye maisha yake yanaendelea tu.
  2. MCHEPUKO VUMBI: Huu ni ule wa vibomu!! mara ooohhh sina pesa, naomba vocha, sijui simu imekufa, oooh mara nipo saluni nadaiwa elf thelathin, naomba nauli…..n.k! Na hii ndio noma maana njia kuu lazima washtuke mana mchepuko vumbi unachafua na unasumbua full time
  3. MCHEPUKO KOKOTO: Huu ni mkali zaidi ya njia kuu maana kila mara huuliza upo wapi, Uko na nani, why hupokei simu yangu? Kama uko kwako naomba utoke nje tuongee kidogo na leo uwe na mimi tu…Yaani tabu tupu! MCHEPUKO MATOPE: Yaani huu usiombe hata kukutana nao maana wenyewe ndio fu
  4. nga kazi.. Huu bana unajua kuchuna hasa ila pale unapoupa pesa na wenyewe unaenda kuzihonga zote kwa mchepuko wake mwingine yaani hatari tupu