Jumatano, 26 Oktoba 2016

YANGA YAIVURUGA JKT RUVU

Siku moja baada ya kocha mkuu wa Dar es salaam young Africa kujiuzulu leo hii likizo hicho kimeondoka na ushindi wa goli nne kwa bila dhidi ya JKT RUVU maafande hawa toka mkoani pwanii. Shukrani zimwendee obrey chirwa aliendelea kuzifumania nyavu pia supersub amisi tambwe akiingia kipindi cha Pili akifunga magoli mawili na saimon msuva akafunga moja.Kwa mchezo huyo simba wanaongoza kwa pointi 29 yanga wanafuatia kwa point 24..

VIKWAZO VYA UJASILIAMALI

Ujasiliamali ni nguzo muhimu katika maendeleo ya watu Popote duniani. Hii ni sekta muhimu ambayo inawezakuleta ajira ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja kwa watu hasa vijana. Kwa Nchi zinazoendelea hasa za Africa sekta hii ni muhimu sana ili kupunguza tatizo la ajira kwa vijana. Nchi nyingi za Africa ina namba kubwa ya vijana wasio na kazi ambapo hupelekea vijana kujiunga na delta zisizo rasmi ili wapate pesa za haraka na kukidhi mahitaji Yao. Je ni nini changamoto zinazowakabili?
  • Kukosekana.kwa mitaji: hili ni.tatizo sugu amabalo hufanya watu wengi washindwe kwenye sekta ya ujasiliamali. Bank na taasisi za kifedha zimekuwa zinatoa masharti magumu ili kupata Mtaji kama uwe na kiwanja ,nyumba na kadhalika.
  • Elimu duni ya ujasiliamali inachangia wale wanothubutu kushindwa kufikia malengo au mafanikio kwa sababu ya elimu duni au mazoea pia ugumu wa maisha hupelekea biashara kutofanikiwa.
  • Starehe vijana wengi wanakumbwa na nanga la.kupenda starehe hivyo hupelekea kipato kuishi kwenda kumbi za starehe , bar na kwenye majumba ya kulala wageni

Jumatano, 12 Oktoba 2016

CHANGAMOTO ZA KILIMO KWA WAKULIMA

Tanzania ni Nchi iliyojaliwa mabonde na ardhi yenye rutuba. Nchi ambayo ina mito mingi mikubwa kama rufiji,malalasi,ruaha n.k pia kuna maziwa makubwa kama Victoria,Nyasa na Tanganyika, hivyo inawezekana kwa kiasi kikubwa shughuli za kilimo zikafanyika mwaka Mzima. Ila wakulima wamekuwa wakipata changamoto nyingi sana ambazo ni:-

  • PEMBEJEO KUCHELEWA AU KUKOSEKANA
      Wakulima wamekuwa wakisotea kupata pembejeo toka serikalini ambapo kwanza hazifiki kwa wakati na zikifika zinakuwa chache kiasi kwamba watu wachache ndo wanaopata. Hili limeshamili sana vijijini huko ambapo wananchi wanalalamika sana suala hili
  • UKOSEFU WA SOKO LA MAZAO
Bei ya mazao imekuwa gonjwa sugu kwani wanunuzi  wamekuwa wakijipangia bei ya kununua mazao bila kujali upande wa mkulima. Hili suala linapelekea mpaka wakulima wanakata tamaa ya kulima mashamba makubwa wakihofia hasara ambayo wanaweza kupata.  Bado matumizi ya jembe la Mkono yanaendelea na kilimo cha kisasa watu wachache sana ndo wanafanya. Hii hupelekea mavuno machache na mazao yasiyo bora.
  • MATUMIZI YA ZANA DUNI ZA KILIMO