Jumamosi, 30 Aprili 2016

MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA ZAHARIBU MIUNDOMBINU YA BARABARA

Kufuatia Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Mtwara zimesababisha wasafiri wanaofanya safari kati ya wilaya ya Tandahimba, Newala, na Dar es Salaam kupata adha kubwa ya usafiri kutokana na barabara kuharibika na kulazimika Magari kuvutwa na Scaveta zinazofanya kazi ya kupunguza mlima kinombedo uliopo wilaya ya Tandahimba.
Wakiwa katika jitihada za kuvuka mlima Kinombedo ambao licha ya kuwepo kwa lami udongo unaoporomoka kutoka juu ya mlima huo umekuwa ukisababisha utelezi na magari kushindwa kupanda mlima ambapo awali madereva wanaoendesha mashine za kuchimbia udongo walishindwa kutoa msaada na kulazimu madereva kuanza kuchimba barabara hali ambayo ilisababisha foleni kubwa zaidi kutokana na malori kuziba njia.
Baada ya jititihada zao kugonga mwamba na kusababisha foleni ya malori ya mizigo pamoja na mabasi ya abiria, Kampuni inayopunguza mlima chini ya msimamizi wake Bw. Haji Abubakari ambaye hakutaka kutaja jina la kampuni inayofanya kazi ilitoa msaada wa kuyavuta magari hayo ambayo baadaye yaliendelea na safari zake , Lakini bwana Haji amesema eneo hilo linapunguzwa mlima ili kuwezesha magari kupita kwa urahisi.
Wakiongea na Safari redio baadhi ya madereva wanaofanya safari zao kati ya Wilaya ya Tandahimba, Newala na Dar es Salaam wameilalamikia serikali ya Mkoa kwa kushindwa kujenga barabra hiyo kwa kiwango cha lami licha ya kuwa imekuwa ina uhitaji mkubwa kwa wananchi wanaoishi na wanaosafiti katika wilaya hizo.
Mmoja wa madereva hao aliyejitambulisha kwa jina na Charles Paulo amesema mara nyingi kipindi cha mvua kumekuwa kukijitokeza kero ya uharibifu wa barabara ambayo kwa namna moja au nyingine imekuwa ikichangia uchakavu wa vyombo vya moto ambavyo vimekuwa vikipita katika barabara hiyo.
Wiki iliyopita Serikali kupitia bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilisema imetenda fedha zaidi ya shilingi Milion 1000 kwa ajili ya kukarabati miundombinu ya barabara na kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayounganisha Mkoa wa Mtwara na Viunga vyake.Kuhu ikidai kuwa serikali kupitia wakala wa barabara Tanroads tayari imesaini mkataba na mkandarasi kutoka Botswana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni